Posts

Showing posts from July, 2020

Urithi utakaoishi alioacha Mkapa

Image
WAKATI Afrika na dunia ikiendelea kumlilia Rais mstaafu Benjamin Mkapa (81) aliyefariki dunia usiku wa kuamkia Julai 24, viongozi mbalimbali wameelezea mchango wake kwa taifa wakisema ni urithi utakaoendelea kuishi baada ya yeye kumaliza safari yake duniani. Mkapa ambaye anatarajiwa kuzikwa kijijini kwake Lupaso Wilaya ya Masasi mkoani Mtwara Juni 29, mbali na marais mbalimbali na viongozi wengine wa kimataifa ambao wameeleza kumkumbuka Mkapa kwa mchango wake wa kidiplomasia, viongozi wengine nchini pia wameeleza mambo ambayo yatazidi kukumbukwa daima. Mkapa aliyeshika nyadhifa mbalimbali kabla ya mwaka 1995 alipokuwa Rais, katika uongozi wake anatajwa kama mtu aliyejenga mifumo ya kitaasisi, kuinua sekta binafsi, kuanzisha taasisi kama Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA), Mfuko wa Bima ya Afya (NHIF), kuanzisha uchimbaji mkubwa wa madini, kuinua diplomasia ya kiuchimi na kuboresha mfumo wa elimu uliosaidia watoto wengi kuanza kuandikishwa shuleni na elimu ya juu. Kwa mujibu wa viongozi m

Serikali ya Tanzania imetangaza kuwa Marehemu Mzee Benjamin William Mkapa atazikwa kijijini kwake Lupaso, wilaya ya Masasi mkoani Mtwara, Kusini mwa Tanzania.

Image
Waziri Mkuu wa Tanzania, Kassim Majaliwa amesema kuanzia siku ya Jumapili, Watanzania wote watapata fursa ya kushiriki shughuli za kuaga zitakazofanyika katika uwanja wa uhuru jijini Dar es Salaam. Shughuli za kumuaga mzee Mkapa zitafanyika kwa siku tatu mfululizo kuanzia tarehe 26 mpaka tarehe 28, kuanzia Jumapili mpaka Jumanne. Siku ya Jumapili kuanzia saa nne asubuhi, Kanisa Katoliki litaongoza misa ambayo wakazi wa Dar es Salaam na nje ya mji huo watapata fursa ya kuaga mwili baada ya misa na zoezi hilo litaendelea siku nzima mpaka siku ya Jumatatu siku nzima pia itatumika kwa shughuli hiyo. Waziri Majaliwa amesema siku ya Jumanne tarehe 28 itakuwa siku ya kuaga kitaifa ambapo viongozi mbalimbali wa serikali nchini , viongozi wa dini, na wananchi. Baada ya zoezi hilo majira ya alasiri mwili wa Kiongozi mstaafu wa taifa hilo utasafirishwa kwenda wilayani Masasi. Mwili wa marehemu utatua katika uwanja wa ndege wa Nachingwea na kutoa fursa kwa wakazi wa eneo hilo kuaga mwili wa marehe

HISTORIA YA BENJAMINI MKAPA.

Benjamin William mkapa, alizaliwa 1938,ana watoto 2, Mkapa ni mhitimu wa Chuo Kikuu cha Makerere. Na Chuo Kikuu cha Columbia Nafasi alizoshikilia zamani ni pamoja na kuwa afisa wa utawala huko Dodoma na Waziri wa Sayansi, Teknolojia na Elimu ya Juu.   Yeye pia aliongoza ujumbe wa Tanzania huko Marekani na alikuwa Waziri wa Mambo ya Nje kutoka 1977 hadi 1980 na kutoka 1984 hadi 1990. Katika mwaka wa 1995, Mkapa alichaguliwa rais msingi wake ukiwa kwa kampeni maarufu ya kupambana na ufisadi na kwa kumuunga mkono kwa nguvu rais wa zamani Julius Nyerere Juhudi za Mkapa za kupambana na ufisadi ni pamoja na kuumba jukwaa la wazi lililoitwa Tume ya Rais juu ya Ufisadi (Tume ya Warioba) na kuongeza msaada kwa Afisi ya Kuzuia Ufisadi,Muhula wa pili wa miaka 5 wa Mkapa kama Rais uliisha Desemba 2005. Katika wakati wake ofisini, Mkapa alibinafsisha makampuni yanayomilikiwa na serikali na akaweka sera za soko huru. Wafuasi wake walimtetea kuwa kuvutia uwekezaji wa kigeni ungesaidia kukuza uchumi.

Rais wa zamani wa Tanzania Benjamin Mkapa, 81, afariki

Image
Aliyekuwa rais wa Tanzania Benjamin Mkapa amefariki. Rais Mkapa aliaga dunia usiku wa kuamkia Ijumaa katika hospitali moja mjini Dar es Salaam. Rais John Magufuli alitangaza kuhusu kifo cha Mkapa, ambaye alikuwa rais wa awamu ya tatu, kupitia taarifa fupi ya moja kwa moja kutoka Ikulu mwendo wa saa sita na dakika ishirini na tano saa za Afrika Mashariki. "Kwa masikitiko makubwa tumepata msiba mkubwa. Mzee wetu, Rais wa awamu ya tatu Benjamin Mkapa amefariki akiwa hospitalini mjini Dar es Salaam ambako alikuwa amelazwa," alisema Rais Magufuli. "Tuendelee kumuombea Mzee Mkapa ambaye ametangulia mbele ya haki," aliongeza. .Kabla ya kuwa rais Mkapa alikuwa miongoni mwa wanadiplomasia waandamizi wa Tanzania akishika nafasi kama waziri wa mambo ya nje na balozi wa Tanzania katika utawala rais wa kwanza Jwa Mwalimu ulius Nyerere na rais wa awamu ya pili Ali Hassan Mwinyi. Wakati wa uongozi wake Mkapa alisifiwa kwa kuweka taratibu na kanuni nyingi za shughuli za kiserikali

TAFAKARI

Siku moja kundi la watu 50 walikuwa wakihudhuria semina moja. Ghafla mwezeshaji akaacha kufundisha na kutoa zoezi ambalo walitakiwa kulifanya kwenye makundi aliyoyagawa. Baada ya hapo akampa kila mtu puto na kumwambia alipulize lijae hewa na kuliandika jina lake kisha wakayakusanya na kuyaweka kwenye chumba kimoja. Walipoyaweka kwenye kile chumba akawapa zoezi la pili kuwa kwa pamoja watumie dakika tano ambapo kila mtu awe amefanikiwa kulitafuta puto lenye jina lake. Waliingia mle ndani kila mtu akawa busy akijaribu kulitafuta puto lake lakini hakuna aliyefanikiwa na dakika tano zaikaisha huku kila mtu akiwa hana puto mkononi. Mwezeshaji akasema tena haya sasa kila mtu aingie na alichukue puto lolote na kumpa mwenye jina lake. Wakaingia na haikufika hata dakika ya nne kila mtu akawa ameshapata puto lake na kakaa kwenye kiti chake. Mwenzeshaji akawaambia hongereni sana, na huu mfano unaendana sana na maisha yetu ya kila siku, ambapo watu wako busy kuitafuta furaha katika maisha yao bila