Posts

Showing posts from June, 2020

UINGEREZA: Hii ndio dawa ya Corona iliyobainika kutibu baada ya majaribio

Image
Shirika la Afya Duniani (WHO) limefurahishwa na matokeo ya awali ya majaribio ya dawa ya kutibu corona Uingereza yanayoonesha kwamba dawa ya dexamethasone, inaweza kuokoa maisha ya watu walio mahututi wanaougua ugonjwa wa Covid-19. Kwa wagonjwa wanaotumia mashine za kupumua, dawa hiyo ilionesha kwamba imepunguza idadi ya vifo kwa theluthi moja, na kwa wagonjwa wanaohitaji hewa ya oksijeni, idadi ya vifo ilipungua kwa humusi au moja ya tano kulingana na matokeo ya awali yaliyotolewa na WHO. Hata hivyo, faida ama uzuri wa dawa hiyo kulijitokeza kwa wagonjwa wanaoumwa sana kwasababu ya virusi vya corona wala sio kwa wenye athari za wastani za ugonjwa huo. Shirika la Afya Duniani (WHO) limefurahishwa na matokeo ya awali ya majaribio ya dawa ya kutibu corona Uingereza yanayoonesha kwamba dawa ya dexamethasone, inaweza kuokoa maisha ya watu walio mahututi wanaougua ugonjwa wa Covid-19. Kwa wagonjwa wanaotumia mashine za kupumua, dawa hiyo ilionesha kwamba imepunguza idadi ya vifo kwa theluth

Maandamano yazuka upya baada ya polisi kumpiga risasi Mmarekani mweusi

Image
Kisa kingine cha polisi nchini Marekani kumpiga risasi na kumuua Mmarekani mwengine mweusi katika mji wa Atlanta Georgia wikendi hii, kimezusha ghadhabu na maandamano tena, pamoja na mjadala unaoendelea ulimwenguni kote wa kupinga ubaguzi wa rangi. Maandamano yazuka upya baada ya polisi kumpiga risasi Mmarekani mweusi Hamza Fumo5 hours ago 259 Kisa kingine cha polisi nchini Marekani kumpiga risasi na kumuua Mmarekani mwengine mweusi katika mji wa Atlanta Georgia wikendi hii, kimezusha ghadhabu na maandamano tena, pamoja na mjadala unaoendelea ulimwenguni kote wa kupinga ubaguzi wa rangi. Man's death after police shooting outside Wendy's in Atlanta ... Mkuu wa polisi wa Atlanta tayari amejiuzulu wadhifa wake kutokana na kisa hicho. Kadhalika idara ya polisi ya Atlanta imesema, imemfuta kazi polisi mmoja kutokana na kifo hicho. Jamaa huyo mwenye umri wa miaka 27 aliyetambuliwa kwa jina Rayshard Brooks alipigwa risasi siku ya Jumamosi, alipokataa kukamatwa baada ya kufeli katika v

UWT DODOMA MJINI YAMUUNGA MKONO RAIS MAGUFULI KWENYE SEKTA YA AFYA NA ELIMU

Image
KATIKA kuunga mkono juhudi za Rais Dk John Magufuli za kuwahudumia watanzania, Umoja wa Wanawake Tanzania (UWT) Wilaya ya Dodoma Mjini umekabidhi vifaa mbalimbali vyenye thamani ya Sh Milioni Mbili kwenye sekta ya Afya na Elimu wilayani humo. Vifaa vilivyotolewa na UWT Wilaya ya Dodoma Mjini ni Mashuka 50 ya kujifunikia katika Kituo cha Afya Mkonze ambacho kilikua kinatumika kuhudumia wagonjwa wenye maambukizi ya ugonjwa wa Corona na vifaa vya kufanyia mitihani katika Shule ya Sekondari Wasichana Msalato. Akizungumza wakati wa kukabidhi vifaa hivyo, Katibu wa UWT Wilaya hiyo, Diana Madukwa amesema juhudi kubwa za kimaendeleo zinazofanywa na Rais Magufuli ndizo ambazo zimewafanya waone kwamba nao wanapaswa kumuunga mkono kwa kuchangia vifaa hivyo. Amesema pia wametoa vifaa hivyo kama pongezi pia kwa Rais Magufuli kwa uwezo wake mkubwa alioonesha katika mapambano dhidi ya Corona ambapo kwa kiasi kikubwa maambuzki yamepungua na shughuli za kimaendeleo zinaendelea kama kawaida. " Tume

Mwili wa George Floyd kuzikwa leo, maelfu wafurika kanisa la ‘The Fountain of Praise’ kutoa heshima za mwisho

Image
George Floyd, Mmarekani mweusi mwenye umri wa miaka 46 ambaye mauaji yake na polisi mweupe yamembadilisha kuwa picha ya ulimwengu ya mapambano dhidi ya ubaguzi wa rangi na ukatili wa polisi, atazikwa leo mjini Houston, ambako alikulia. Waombolezaji wengi walitengeneza ishara ya msalaba wakati wakikaribia jeneza la Floyd lililokuwa wazi, katika kanisa la The Fountain of Praise mjini Houston, jimbo la Texas, kutoa heshima zao za mwisho wakati wengine wakipiga magoti au kuinamisha vichwa na kumuombea kimyakimya mtu ambaye amekuwa ishara ya karibuni ya vuguvugu la kupinga ubaguzi wa rangi Marekani. Mwili wa George Floyd kuzikwa leo, maelfu wafurika kanisa la ‘The Fountain of Praise’ kutoa heshima za mwisho (+Picha) Hamza Fumo6 hours ago 343 George Floyd, Mmarekani mweusi mwenye umri wa miaka 46 ambaye mauaji yake na polisi mweupe yamembadilisha kuwa picha ya ulimwengu ya mapambano dhidi ya ubaguzi wa rangi na ukatili wa polisi, atazikwa leo mjini Houston, ambako alikulia. Public viewing fo

Rais Magufuli: Ugonjwa wa Corona nchini umeondolewa kwa nguvu za Mungu

Image
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Dkt. John Pombe Magufuli amewashukuru viongozi wa dini na Watanzania wote kwa kuitikia wito wa kumuomba Mungu aepushe janga la ugonjwa wa homa ya mapafu unaosababishwa na virusi vya Corona (Covid-19). Rais Magufuli amesema Mungu amejibu maombi ya Watanzania ambao wamesali, wamefanya toba na kufunga, na matokeo yake ni kuwa maambukizi ya virusi vya Corona yamepungua, na wananchi wanaendelea na maisha yao huku wakichapa kazi za uzalishaji mali, tofauti na ilivyodhaniwa kuwa ugonjwa huo ungesababisha madhara makubwa. Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Dkt. John Pombe Magufuli akizungumza wakati alipokuwa akiendesha Harambee ya Papo kwa papo kwa ajili ya upanuzi wa Kanisa Katoliki Parokia ya Mtakatifu Bikira Maria Imaculata Chamwino Ikulu mkoani Dodoma leo tarehe 7 Juni 2020. Katika Harambee hiyo jumla ya Shilingi Milioni 17 zilipatikana pamoja na mifuko 76 ya Saruji na Mhe. Rais Magufuli alichanga peke yake kiasi cha Shili

Zanzibar waruhusu ndege za kitalii kuanza kutua

Image
Serikal ya Mapinduzi ya Zanzibar imeruhusu kuanzia leo safari za ndege za kitalii kuwasili nchini baada ya mambukizi ya virusi vya Corona kupungua. Taarifa hiyo imetolewa hivi punde na Waziri wa Habari Utalii na Mambo ya Kale Mahmood Thabit Kombo ambapo amesema serikali imefikia uwamuzi huo baada ya kujiridhisha na kiasi kidogo cha maambukizi ya corona. Waziri Kombo ameeleza pamoja na serikali kuruhusu shughuli za utalii kuendelea ni vyema shughuli hizo zikaendeshwa kwa kuzingatia tahadhari ya virusi vya corona kwa wageni kupimwa kila wanapoingia nchini, na wageni wote kutakiwa kuwa na bima zao za afya kabla hawajingia nchini.

Waombolezaji watoa heshima za mwisho, watumia sekunde 46 muda ambao Floyd alivumilia chini ya goti la polisi

Image
Quincy Mason Floyd ambaye ni mtoto wa marehemu George Floyd Mmarekani mwenye asili ya Afrika aliyefariki dunia mikononi mwa polisi amewashukuru watu wote waliojumuika na familia yao katika kuwafariji kupitia kipindi hiki wanachopitia. Quincy Mason Floyd (akiwa kati alipozuru eneo ambalo baba yake mzazi George Floyd aliuawa) Hayo ameyasema wakati maelfu ya watu wakiwa wamekusanyika katika kutoa heshima zao za mwisho “Ninamshukuru kila mmoja wenu aliyekuja kutufariji wakati huu mgumu wa msiba wa baba yangu.” Quincy Mason Floyd Waombolezaji waliokusanyika kutoa heshima zao walikaa kimya kwa dakika nane, sekunde 46, muda ambao Floyd alivumilia chini ya goti la polisi mjini Minneapolis hadi akapoteza fahamu. Duru zinasema kuwa marehemu George Floyd alikuwa na ugonjwa wa Corona . . . ” Si janga la corona lililomuua George Floyd”. ”Janga la ubaguzi wa rangi limemuua Floyd.” Wakili wa familia ya Floyd, bw Benjamin Crump aliwaambia waombolezaji walihudhuria ibada ya kumkumbuka mtu mweusi aliye

Wanigeria wataka haki itendeke kwa mwananfunzi aliyebakwa na kupoteza maisha wakati akijisomea kanisani

Image
Kuna ghadhabu nchini Nigeria baada ya mauaji ya mwanafunzi mwenye umri wa miaka 22, Uwavera Omozuwa aliyeuawa kanisani. Wanigeria wataka haki itendeke kwa mwananfunzi aliyebakwa na kupoteza maisha wakati akijisomea kanisani Ally Juma1 hour ago 237 Kuna ghadhabu nchini Nigeria baada ya mauaji ya mwanafunzi mwenye umri wa miaka 22, Uwavera Omozuwa aliyeuawa kanisani. Kampeni ya hashtag #JusticeForUwa au # HakiKwaUwa imeenea kwenye mitandao ya kijamii nchini Nigeria, huku familia yake ikiomba msaada wa kumtafuta aliemuua. Uwavera alikua anajisomea katika kanisa “tulivu” karibu na nyumbani Benin City wakati alipouawa, dada yake, Judith, aliiambia BBC kuwa. Mwanafunzi huyo ambaye alikuwa na ndoto ya kuwa muuguzi alikufa hospitalini siku ya Jumamosi, siku tatu baada kushambuliwa. Judith Omozuwa alisema kuwa dada yake alibakwa. Familia yake ilisema kuwa ilipokea simu kutoka kwa mwanamke kutoka kanisa la Redeemed Christian Church of God siku ya Jumatano jioni. Uwavera alipelekwa hospitalini ba