Waombolezaji watoa heshima za mwisho, watumia sekunde 46 muda ambao Floyd alivumilia chini ya goti la polisi

Quincy Mason Floyd ambaye ni mtoto wa marehemu George Floyd Mmarekani mwenye asili ya Afrika aliyefariki dunia mikononi mwa polisi amewashukuru watu wote waliojumuika na familia yao katika kuwafariji kupitia kipindi hiki wanachopitia.
Quincy Mason Floyd (akiwa kati alipozuru eneo ambalo baba yake mzazi George Floyd aliuawa)

Hayo ameyasema wakati maelfu ya watu wakiwa wamekusanyika katika kutoa heshima zao za mwisho “Ninamshukuru kila mmoja wenu aliyekuja kutufariji wakati huu mgumu wa msiba wa baba yangu.” Quincy Mason Floyd

Waombolezaji waliokusanyika kutoa heshima zao walikaa kimya kwa dakika nane, sekunde 46, muda ambao Floyd alivumilia chini ya goti la polisi mjini Minneapolis hadi akapoteza fahamu.
Duru zinasema kuwa marehemu George Floyd alikuwa na ugonjwa wa Corona . . . ” Si janga la corona lililomuua George Floyd”. ”Janga la ubaguzi wa rangi limemuua Floyd.” Wakili wa familia ya Floyd, bw Benjamin Crump aliwaambia waombolezaji walihudhuria ibada ya kumkumbuka mtu mweusi aliyeuawa tarehe 25 mikononi mwa polisi mzungu aliyechomeka goti kwenye shingo lake.

Comments

Popular posts from this blog

HISTORIA YA MKWAWA AMBAYE ALIWAHI KUWA CHIFU WA UHEHE HISTORIA YA MKWAWA Mkwawa alikuwa kiomgozi wa jadi wa kabila la wahehe nchini Tanzania, ni moja kati ya viongozi shupavu wa jadi waliowahi kuishi duniani japo mapokeo yao yanaharibiwa taratibu na mabadiliko ya sayansi na technolojia lakini kumbukumbu zao hazitasahauliki hata vizazi vingi vijavyo. miongoni mwa machifu wanaotajwa kuwa na nguvu za kiutawala kwa kipindi hicho ni pamoja na kinjekitile ngwale wa songea aliyeongoza vita za majimaji, Mirambo wa Tabora nk PICHA YA MKWAWA

Nigeria, Rwanda ruksa kutoka nje, ni baada ya Lockdown

Mwili wa George Floyd kuzikwa leo, maelfu wafurika kanisa la ‘The Fountain of Praise’ kutoa heshima za mwisho