Nigeria, Rwanda ruksa kutoka nje, ni baada ya Lockdown

Nchi za Rwanda na Nigeria kuanzia leo Jumatatu zimeanza kulegeza masharti ya amri ya kusalia ndani kwa wananchi wake kama sehemu ya mapambano dhidi ya corona.


Nchini Rwanda marufuku hiyo ilikuwa imewekwa nchi nzima, huku Nigeria marufuku hiyo ilihusisha ndani katika mji mkuu wa Abuja, na mji mkubwa kabisa wa Lagos, katika jaribio la kupunguza athari ya kiuchumi barani Afrika.

Nchi hizo mbili, zinaungana na mataifa mengine ya Afrika kama Ghana, Afrika Kusini na Kenya ambayo pia yamelegeza baadhi ya masharti makali ya hatua hizo za watu kusalia ndani.

Mataifa kadhaa ya Afrika yamechukua hatua ya kuweka marufuku hiyo toka mlipuko wa virusi hivyo kuingia barani na kuonesha hatari ya maambukizi ya ndani ya jamii.

Uganda pia inatarajiwa kutangaza kulegeza masharti kesho. Raisi Museveni anatarajiwa kulihutubia taifa hilo jioni ya leo.

Baadhi ya shughuli za kibiashara zinatarajiwa kufunguliwa japo shule zinatarajiwa kuendelea kufungwa mpaka hapo itakapotangazwa.
Japo hatari ya virusi ingalipo, nchi za Afrika zinalegeza masharti na kuonekana kukabiliana vyema na virusi.

Comments

Popular posts from this blog

HISTORIA YA MKWAWA AMBAYE ALIWAHI KUWA CHIFU WA UHEHE HISTORIA YA MKWAWA Mkwawa alikuwa kiomgozi wa jadi wa kabila la wahehe nchini Tanzania, ni moja kati ya viongozi shupavu wa jadi waliowahi kuishi duniani japo mapokeo yao yanaharibiwa taratibu na mabadiliko ya sayansi na technolojia lakini kumbukumbu zao hazitasahauliki hata vizazi vingi vijavyo. miongoni mwa machifu wanaotajwa kuwa na nguvu za kiutawala kwa kipindi hicho ni pamoja na kinjekitile ngwale wa songea aliyeongoza vita za majimaji, Mirambo wa Tabora nk PICHA YA MKWAWA

Mwili wa George Floyd kuzikwa leo, maelfu wafurika kanisa la ‘The Fountain of Praise’ kutoa heshima za mwisho