HISTORIA YA OSAMA BIN LADEN KUZALIWA MPAKA KUFA



Osama bin Mohammed bin Awad bin Laden alizaliwa Riyadh huko Saud Arabia katika famila ya ndugu Mohammed bin Awad bin Laden ambaye alikuwa ni tajiri mkubwa sana kwa nyakati hizo utajiri ambao aliupata kwa kazi yake ya ukandarasi, Osama bin Laden alizaliwa 10,march, 1957 kwa Hamida al-Attas alikuwa mke wa kumi katika orodha ya wake za baba yake Mohammed na ambaye alimpa taraka muda mfupi baada ya Osama kuzaliwa, Hivyo watoto aliozaliwa tumbo moja na Osama walikuwa jumla yao wanne akiwepo mwanamke mmoja ambaye ni dada yao. ELIMU Osama amehudhuria shule Al-Thager model school, na baadaye akahudhuria masomo ya Uchumi na biashara katika chuo cha KING ABDULAZIZ. Lakini pia alikuwa na shahada ya ufundi na ya maendeleo ya jamii. Ukweli ni kuwa alikuwa ni mtu aliyekuwa ni mtu mwenye bidii katika kila jambo au kazi, pamoja na hayo yote Osama aliipenda sana dini yake kupindukia kama walivyo waarabu wengine wenye itikadi kali, muda mwingi aliutumia kuichambua quran na kazi za kujitolea. Osama alipendelea pia kuandika hadithi mbalimbali, kusoma vitabu vya baadhi ya waandishi kama FIELD MARSHAL BERNAD MONTGOMERY na CHARLES DE GAULLE, na akawa vilevile mpenzi wa mpira wa miguu ambapo alicheza fowadi ya katika kati na timu aliyokuwa mshabiki ni ARSENAL FC MAISHA BINAFSI Mnamo mwaka 1974 akiwa na umri wa miaka 17 Osama aliingia kwenye maisha ya ndoa rasmi ambapo ali mwoa Najwa Ghanem huko Latakia Siria ambaye walikuja kutengana kabla ya sept 11, 2001. Baadhi ya wa ke zake walijulikana ni Khadijah Sharif aliyemuoa 1983 na akampa talaka 1990, Khairian Sabar aliyemuoa 1985, Siham Sar aliyemuoa 1987 na Amal al-Sadah aliyemuoa 2000, inasadikika kuwa ni baba wa watoto kati ya 20 mpaka 26 kwa wake zake wote. Watoto wake wengi walikimbilia Iran baada ya mashambulizi ya baba yao ya sept 11 na 2010. mamlaka husika huko Iran zinataja kuwa bado zinaendelea kudhibiti mien endo yao. Mwanae mmoja wa kiume na ambaye alikuwa ni bodyguard wake anaeleza kuwa baba yake ali kuwa ni mtu mtafiti sana mkali kupindukia japo aliipenda sana familia yake na alikuwa na kawaida ya kuitoa familia yake nje kutalii na kustarehe kwenye fukwe mbalimbalil Baba yake Osama bin Laden alifariki 1967 kwa ajali ya ndege Saud Arabia, pia kaka yake Salem bin laden aliuawawa San Antonio huko Texas USA IMANI YAKE Osama bin Laden alikuwa akiaminia kuwa marekani wanawachukia sana waislam sio kwa sababu ya jinsi walivyo bali kwa sababu ya yale wanayotenda, pia akaongeza kuwa ni sheria ya SHARIA pekee ndiyo ita kayowaweka huru toka kwenye unyanyasaji wa marekani kwenye ulimwengu wa kiislam, na bado aliamini kuwa Afganistan chini ya utawala wa Mullah Omars Taliban ndiyo nchi pekee ya kiislam Duniani, bado alikuwa na mpango wa kuiangamiza Israel na kuilazimisha marekani kuiachia mashariki ya kati MAISHA YAKE JESHINI Baada ya kuhitimu elimu yake ya chuo, Osama alikwenda pakistani ambako alitumia fedha na mali zake za urithi katika kumsaidia Abdullah Azzam ambaye alikuwa na jeshi lililokuwa likipinga vita ya kisoviet huko Afganistan, TUKUTANE TENA KWENYE SEHEMU INAYOFUATA KUHUSU MAISHA YAKE JESHINI MPAKA KIFO CHAKE OSAMA BIN LADEN
By
    Shyzzoh

Comments

Popular posts from this blog

HISTORIA YA MKWAWA AMBAYE ALIWAHI KUWA CHIFU WA UHEHE HISTORIA YA MKWAWA Mkwawa alikuwa kiomgozi wa jadi wa kabila la wahehe nchini Tanzania, ni moja kati ya viongozi shupavu wa jadi waliowahi kuishi duniani japo mapokeo yao yanaharibiwa taratibu na mabadiliko ya sayansi na technolojia lakini kumbukumbu zao hazitasahauliki hata vizazi vingi vijavyo. miongoni mwa machifu wanaotajwa kuwa na nguvu za kiutawala kwa kipindi hicho ni pamoja na kinjekitile ngwale wa songea aliyeongoza vita za majimaji, Mirambo wa Tabora nk PICHA YA MKWAWA

Nigeria, Rwanda ruksa kutoka nje, ni baada ya Lockdown

Mwili wa George Floyd kuzikwa leo, maelfu wafurika kanisa la ‘The Fountain of Praise’ kutoa heshima za mwisho