Tanzania vs Tunisia, tuiombe Taifa Stars – Rais TFF Wallace Karia.

Rais wa Baraza la Soka Afrika Mashariki na Kati Cecafa na ambaye ni Rais wa Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF) Wallace Karia amewaomba Watanzania kuiombea timu ya taifa ya Tanzania maarufu kama Taifa Stars kuhakikisha hii leo usiku inachomoza na ushindi dhidi ya Tunisia kwenye mchezo wa ‘Group J’ mchezo wa kufuzu AFCON 2021 utakaopigwa uwanja wa Mkapa saa 4:00 usiku.


Karia ambaye pia ni Rais wa Baraza la Soka Afrika Mashariki na Kati Cecafa amezungumzia mashindano ya Cecafa ya U20 yatakayoanza kutimua vumbi tarehe 22 katika Mkoa wa Arusha na Karatu nchini Tanzania.

Mashindano hayo yanatarajiwa kufikia tamati tarehe 2 Disemba na kushirikisha jumla ya timu tisa (9).

Wallace Karia amesema dhana yake ni kuhakikisha ausambaza mchezo wa mpira wa miguu katika sehemu mbalimbali.



”Matarajio yangu katika kipindi changu tutaziacha timu zikiwa juu katika Rank ya FIFA tofauti tunavyotazamwa sasa hivi ziko chini. Tulichukua U17 Boys, mwaka jana tukachukua U20 Girls na mwaka huu tumekwenda kuchukua U17 Girls kwa hiyo timu zetu zinafanya vizuri.”

Comments

Popular posts from this blog

HISTORIA YA MKWAWA AMBAYE ALIWAHI KUWA CHIFU WA UHEHE HISTORIA YA MKWAWA Mkwawa alikuwa kiomgozi wa jadi wa kabila la wahehe nchini Tanzania, ni moja kati ya viongozi shupavu wa jadi waliowahi kuishi duniani japo mapokeo yao yanaharibiwa taratibu na mabadiliko ya sayansi na technolojia lakini kumbukumbu zao hazitasahauliki hata vizazi vingi vijavyo. miongoni mwa machifu wanaotajwa kuwa na nguvu za kiutawala kwa kipindi hicho ni pamoja na kinjekitile ngwale wa songea aliyeongoza vita za majimaji, Mirambo wa Tabora nk PICHA YA MKWAWA

Nigeria, Rwanda ruksa kutoka nje, ni baada ya Lockdown

Mwili wa George Floyd kuzikwa leo, maelfu wafurika kanisa la ‘The Fountain of Praise’ kutoa heshima za mwisho