Virusi vya corona: Mtaalamu wa chanjo 'aliyefutwa kazi' asema Marekani itakabiliwa na hali mbaya zaidi katika majira ya baridi


Afisa wa zamani wa ngazi ya juu wa afya nchini Marekani ameliambia bunge la kongresi kuwa nchi inaweza kukabiliwa na "kipindi kibaya zaidi cha majira ya baridi kuwahi kushuhudiwa katika historia ya hivi karibuni " kwa sababu ya virusi vya corona.

Rick Bright aliongoza shirika la serikali kujaribu kutengeneza chanjo,lakini akaondolewa katika kazi hiyo mwezi uliopita.

Awali alisema aliondolewa kazini kwa kuelezea hofu juu ya tiba zinazotangazwa na rais Donal Trump.

Rais Trump alimfuta kazi kwa madai kuwa alikua mtumishi "asiyeridhika"

Bwana Bright pia aliiambia kamati ya Bunge la wawakilishi ya masuala ya afya kuwa ''maisha yanapotea'' kwa sababu ya serikali "kutochukua hatua " katika hatua za mwanzo za mlipuko wa virusi vya corona.

Alisema kuwa kwa mara ya kwanza alizungumzia juu ya ukosefu wa zana za matibabu mwezi Januari, na kufikisha suala hilo katika "ngazi za juu" za Wizara ya Afya na huduma za binadamu (HHS), lakini "hakujibiwa".

Ni nini kingine alichosema Bwana Bright ?
Wakati wa ushahidi, Bwana Bright alionya kwamba " dirisha " la kushughulikia virusi vya corona linakaribia "kufunga".

"Kama tutashindwa kuboresha jinsi tunavyokabiliana na ugonjwa huu sasa, kwa misingi ya sayansi, ninaogopajanga litakua baya sana na kuendelea kwa muda mrefu ," alisema.

"Bila mpango bora, 2020 unaweza kuwa na kipindi kibaya zaidi cha majira ya baridi kuwahi kushuhudiwa katika histioria ya sasa ."

Bwana Bright pia ameiambia kamati hiyo ya bunge la wawakilishi kuwa mwezi Januari alipokea barua pepe ambayo "hawezi kusahau ", kutoka kwa wasambazaji wa barakoa za hospitali ambao walioonya juu ya upungufu mkubwa wa barakoa,

"Alisema... tunahitaji kuchukua hatua.Na nikaituma barua hiyo kwa ngazi ya juu ya HHS - na sikupata jibu."

Comments

Popular posts from this blog

HISTORIA YA MKWAWA AMBAYE ALIWAHI KUWA CHIFU WA UHEHE HISTORIA YA MKWAWA Mkwawa alikuwa kiomgozi wa jadi wa kabila la wahehe nchini Tanzania, ni moja kati ya viongozi shupavu wa jadi waliowahi kuishi duniani japo mapokeo yao yanaharibiwa taratibu na mabadiliko ya sayansi na technolojia lakini kumbukumbu zao hazitasahauliki hata vizazi vingi vijavyo. miongoni mwa machifu wanaotajwa kuwa na nguvu za kiutawala kwa kipindi hicho ni pamoja na kinjekitile ngwale wa songea aliyeongoza vita za majimaji, Mirambo wa Tabora nk PICHA YA MKWAWA

Nigeria, Rwanda ruksa kutoka nje, ni baada ya Lockdown

Mwili wa George Floyd kuzikwa leo, maelfu wafurika kanisa la ‘The Fountain of Praise’ kutoa heshima za mwisho