TDiamond aanza kutimiza ahadi ya kuzilipia familia 500 kodi kwa miezi 3, Familia 57 zanufaika bado 443

Msanii na Mkurugenzi wa Kampuni ya Wasafi, Naseeb Abdul maarufu ‘Diamond Platnumz’ ametoa msaada wa kodi ya pango kwa watu 57 ambao ni Wajane, Walemavu pamoja na Wasiojiweza.
Msaada huo ni awamu ya kwanza katika dhamira yake ya kusaidia kodi ya pango kwa Kaya 500 nchini zilizoathirika kiuchumi na janga la #CoronaVirus.

Diamond ametoa msaada huo siku ya Jumatatu ya tarehe 4/5/2020 katika Makao Makuu ya Kampuni ya WasafiMedia baada ya watu zaidi ya 100 kujitokeza ofisini hapo ambapo familia 57 zimeweza kupata msaada huo.
Kwa Familia 443 zilizobaki bado mchakato unaendelea kwa ajili ya kuzipatia msaada huo.

Comments

Popular posts from this blog

HISTORIA YA MKWAWA AMBAYE ALIWAHI KUWA CHIFU WA UHEHE HISTORIA YA MKWAWA Mkwawa alikuwa kiomgozi wa jadi wa kabila la wahehe nchini Tanzania, ni moja kati ya viongozi shupavu wa jadi waliowahi kuishi duniani japo mapokeo yao yanaharibiwa taratibu na mabadiliko ya sayansi na technolojia lakini kumbukumbu zao hazitasahauliki hata vizazi vingi vijavyo. miongoni mwa machifu wanaotajwa kuwa na nguvu za kiutawala kwa kipindi hicho ni pamoja na kinjekitile ngwale wa songea aliyeongoza vita za majimaji, Mirambo wa Tabora nk PICHA YA MKWAWA

Nigeria, Rwanda ruksa kutoka nje, ni baada ya Lockdown

Mwili wa George Floyd kuzikwa leo, maelfu wafurika kanisa la ‘The Fountain of Praise’ kutoa heshima za mwisho