Bundesliga kuanza kutimua vumbi kesho, Dortmund kuwavaa Shalke 04

Ligi kuu ya kandanda ya Ujerumani, Bundesliga, inarejea tena mwishoni mwa juma baada kusitishwa kwa karibu miezi miwili kutokana na janga la virusi vya corona.
Kuanza tena kwa ligi hiyo kunaangaliwa kama jaribio juu ya iwapo kandanda na mashindano mengine ya michezo duniani yanaweza kuanza tena chini ya kiwingu cha janga la COVID-19.

Miongoni mwa michezo ya kufungua dimba itayofanyika kesho ni pamoja na mpambano wa kukata na shoka kati ya mahasimu wa jadi Borussia Dortmund na Shalke 04 mjini Dortmund.

Hata hivyo mechi tisa za duru ya 26 ya Bundesliga zitachezwa bila kuwepo mashabiki uwanjani. Ligi nyingine barani Ulaya ikiwemo ile ya Uingereza, Italia na Uhispania zinatarajiwa kuanza tena baadae mwezi Juni.

Comments

Popular posts from this blog

HISTORIA YA MKWAWA AMBAYE ALIWAHI KUWA CHIFU WA UHEHE HISTORIA YA MKWAWA Mkwawa alikuwa kiomgozi wa jadi wa kabila la wahehe nchini Tanzania, ni moja kati ya viongozi shupavu wa jadi waliowahi kuishi duniani japo mapokeo yao yanaharibiwa taratibu na mabadiliko ya sayansi na technolojia lakini kumbukumbu zao hazitasahauliki hata vizazi vingi vijavyo. miongoni mwa machifu wanaotajwa kuwa na nguvu za kiutawala kwa kipindi hicho ni pamoja na kinjekitile ngwale wa songea aliyeongoza vita za majimaji, Mirambo wa Tabora nk PICHA YA MKWAWA

Nigeria, Rwanda ruksa kutoka nje, ni baada ya Lockdown

Mwili wa George Floyd kuzikwa leo, maelfu wafurika kanisa la ‘The Fountain of Praise’ kutoa heshima za mwisho