Waislamu waanza mfungo wa mwezi wa Ramadhan

Waislamu kote ulimwenguni wanaanza ibada ya mfungo wa mwezi mtukufu wa Ramadhan, katikati ya sintofahamu inayotokana na hatua za kukabiliana na kusambaa kwa virusi vya corona ambazo ni Pamoja na kuwazuia watu kutoka nje.


Waislam waanza mfungo wa mwezi wa Ramadhan

Virusi vya corona kwa kiasi kikubwa vimebadilisha mfumo wa Maisha duniani, huku mataifa yakipambana kwa kila hali kukabiliana na maradhi yanayosababishwa na virusi hivyo vinavyosababisha ugonjwa wa COVID19. Karibu vifo 190,000 vimetokea kutokana na ugonjwa huo, idadi ya walioambukizwa hivi sasa inakaribia milioni 2.7, na pia uchumi wa dunia umeathirika pakubwa.

Waumini wa dini ya Kiislamu kuanzia Kusini Mashariki mwa Asia hadi Mashariki ya Kati na hata Afrika wanaanza mwezi huu mtukufu katikati kadhia ya mapambano haya, kwa kuzuiwa kukusanyika na hata kutoka nje.

Hawaruhusiwi kukusanyika kwa ibada misikitini na hata kufanya mikusanyiko mikubwa ya kifamilia pamoja na marafiki wakati wa futari nyakati za jioni baada ya siku nzima ya mfungo, kama ilivyozoeleka.

Hata hivyo licha ya kitisho kinacholetwa na virusi vya corona, viongozi wa dini na wahafidhina katika mataifa mengi kama Bangladesh, Pakistan na Indonesia ambayo yanakaliwa na idadi kubwa ya Waislamu, wanapuuzilia mbali sheria za kutokukusanyika na kuendelea kwenda misikitini.

Maelfu ya watu walihudhuria ibada ya jioni jana Alhamisi iliyofanyika kwenye msikiti mkubwa uliopo kwenye mji mkuu wa Indonesia na kulishuhudiwa mikusanyiko kama hiyo katika maeneo mengi nchini Pakistan.

Comments

Popular posts from this blog

HISTORIA YA MKWAWA AMBAYE ALIWAHI KUWA CHIFU WA UHEHE HISTORIA YA MKWAWA Mkwawa alikuwa kiomgozi wa jadi wa kabila la wahehe nchini Tanzania, ni moja kati ya viongozi shupavu wa jadi waliowahi kuishi duniani japo mapokeo yao yanaharibiwa taratibu na mabadiliko ya sayansi na technolojia lakini kumbukumbu zao hazitasahauliki hata vizazi vingi vijavyo. miongoni mwa machifu wanaotajwa kuwa na nguvu za kiutawala kwa kipindi hicho ni pamoja na kinjekitile ngwale wa songea aliyeongoza vita za majimaji, Mirambo wa Tabora nk PICHA YA MKWAWA

Nigeria, Rwanda ruksa kutoka nje, ni baada ya Lockdown

Mwili wa George Floyd kuzikwa leo, maelfu wafurika kanisa la ‘The Fountain of Praise’ kutoa heshima za mwisho