Mfahamu Irrfan Khan, Mcheza filamu maarufu India aliyepoteza maisha

Muigizaji huyo maarufu kutoka tasnia ya filamu za Kihindi (Bollywood) aliyetamba katika filamu za ‘Slumdog Millionaire’ na ‘Jurassic World’ amefariki leo asubuhi akiwa na miaka 53.
Mwaka 2018, alitangaza kuwa na saratani katika mfumo wa tezi zinazotengeneza homoni (Endocrine Tumour). Tangu jana amekuwa kwenye Chumba cha Uangalizi Maalumu (ICU) hospitali kutokana na bakteria kwenye utumbo ‘Colon Infection’.

Mwaka 2013, alishinda tuzo ya Kitaifa ya Filamu za India kutokana na filamu ya Paan Singh Tomar. Filamu nyingine alizotamba nazo ni Lunchbox, The Namesake, New York, I Love You na Hindi Medium. Ya mwisho, Angrezi Medium imetoka mwezi uliopita.

Khan amezikwa katika makaburi ya Versova Kabristan huko Mumbai muda mfupi baada ya taarifa zake za kifo kutolewa. Familia, ndugu na marafiki wa karibu ndio wamehudhuria.

Comments

Popular posts from this blog

HISTORIA YA MKWAWA AMBAYE ALIWAHI KUWA CHIFU WA UHEHE HISTORIA YA MKWAWA Mkwawa alikuwa kiomgozi wa jadi wa kabila la wahehe nchini Tanzania, ni moja kati ya viongozi shupavu wa jadi waliowahi kuishi duniani japo mapokeo yao yanaharibiwa taratibu na mabadiliko ya sayansi na technolojia lakini kumbukumbu zao hazitasahauliki hata vizazi vingi vijavyo. miongoni mwa machifu wanaotajwa kuwa na nguvu za kiutawala kwa kipindi hicho ni pamoja na kinjekitile ngwale wa songea aliyeongoza vita za majimaji, Mirambo wa Tabora nk PICHA YA MKWAWA

Nigeria, Rwanda ruksa kutoka nje, ni baada ya Lockdown

Mwili wa George Floyd kuzikwa leo, maelfu wafurika kanisa la ‘The Fountain of Praise’ kutoa heshima za mwisho